Mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka
65 kutoka Berlin Ujerumani ambaye ana watoto kumi na watatu ametangaza
kuwa ni mja mzito na pacha wanne.
Kwa mwaka mmoja unusu sasa , bi
Annegret Raunigk ambaye ni mwalimu wa kingereza na kirusi amekuwa
akijaribu kupata mtoto mwingine kwa njia ya upandikizaji,
Kulingana na vyombo vya habari vya German RTL.
Bibi
huyo anasema kuwa alilazimika kuwatafuta watoto zaidi baada ya kitinda
mimba wake mwenye umri wa miaka 9 kumsihi umtafutia watoto atakaocheza
nao.
Bi Raunigk, ambaye amebeba mimba hiyo kwa majuma 21 sasa
anasema kuwa alishtuka kujua kuwa alikuwa amejaaliwa mimba ya watoto 4
wala sio mmoja kama alivyotarajiwa


Post a Comment