Zaidi ya watu 1000
wamekufa kwa tetemeko la ardhi nchini Nepal.
Tetemeko hilo
lililopiga mji wa Kathmandu na Pokhara
na nguvu ya kipimo cha 7.8 magnitude kwa nguvu lilitikisa pia India,
Bangladesh, Tibet na mlima Everest.
Serikali
imetangaza hali ya hatari na kuanza kukimbiza misaada maeneo yaliyovurugika
vibaya.
Kwa mujibu wa
televisheni ya CNN kitovu cha tetemeko kilikuwa maili 50 kutoka mji mkuu wa
Nepal wa Kathmandu.
Imeelezwa kuwa
majengo mengi ya kihistoria mjini Kathmandu yameharibiwa na mpaka usiku wa
jumamosi matememeko madogo yaliendelea kutikisa na kuleta hofu zaidi. Watu wa
jiolojia wa Marekani ambao hufanyakazi ya kuangalia matetemeko duniani wamesema kwamba kumekuwa na matetemeko madogo
15 ya magnitude 4.5 na mengine yalikuwa ya 6.6 na 5.1.
Katika nchi jirani
China maeneo ya Tibet, majengo yameanguka na watu 12 wamekufa.
Moja ya maeneo ya
kihistoria yaliyobomoka ni mnara wa Dharahara ambao pia unajulikana kama
Bhimsen Tower umeporomoka.Mnara huo uliojengwa mwaka 1832, ulikuwa na urefu wa
mita 60 sawa na futi 200 na ulikuwa unatumika kuangalia bonde la Kathmandu .
CNN imesema kwamba
tetemeko hilo ni kubwa la kwanza kwa takribani mikaa 80. Mwaka 1934 Nepal
ilipigwa na tetemeko la 8.1 na kuua zaidi ya watu 10,000.





Post a Comment